123 MWOKOZI mzuri ninaye

123

1. Mwokozi mzuri ninaye, zamani sikumfahamu, na sasa ninamhubiri, wengine wapate kuona.

Pambio:
Wote watamwona, wote watamwona Mwokozi mzuri ninaye; Lo! Wote watamwona.

 

2. Shetani akinizuia nisimfuate Mwokozi, najua Bwanangu hodari hutaka kunisaidia.

 

3. Apita wo wote kwa wema, mfano ‘tukufu wa Baba, lakini anitaja ndugu, niliye maskini kabisa.

 

4.Natoa maisha na pendo kwa Yesu aliyenipenda. Katika ishara za Mungu upendo wapita yo yote.

Carrie E. Breek, 1902
I have such a wonderful Saviour, R.H. 640