191 YAPIGWA hodi kwangu
191
1. Yapigwa hodi kwangu, mgeni a’fika, akiniomba: “Nifungulie! Umande umeshuka kichwani usiku, na nywele zangu zimelowa maji”.
2. A! Huyu si mgeni, ni Yesu Mwokozi, sauti yake nzuri na’jua. Ninamfungulia, naona ni Yesu; na siku hiyo sitaisahau.
3. Anong’oneza sasa rohoni: “U wangu”, karibu naye ninatulia. Ananitia nguvu, baraka ya mbingu; daima nitakaa kwake Yesu.
4. Ni kweli, mimi ni wa Mwokozi milele, amenitaja: “Ndugu, mpenzi”. Ananikarimia hazina za mbingu, ninaingoja siku ya arusi.
Fr. Schibboleth. arr L.P