23 NIKITAZAMA kwa imani Mwokozi wangu

23

1. NIKITAZAMA kwa imani, Mwokozi wangu, Yesu, Nawaka kwa upendo wake, Na ninavutwa kwake; Naona majeraha yake, Mikono na ubavu wake, Na humo najificha sana, Moyoni mwa upendo

 

2. Imanuel upendwaye, Nilinde sikuzote, Mpaka nihamie kwako Mbinguni mwa uheri! Milele na milele huko hapana la kunizuia Nimsifu Bwana Yesu kwa damu na ‘jereha.