6 TWA’SIFU Mungu kwa ajili ya damu takatifu

 1. Twa’sifu Mungu kwa ajili ya damu takatifu,
Inayotosha kuonda makosa yetu yote. [br] 

2.Wakristo wanakusanyika karibu ya kisima,
hawapunguki kitu kanwe, wakaa kwa Mwokozi. [br] 

3. Tuimbe duniani pote juu ya pendo kubwa, 
kwa kuwa tumefunguliwa kisima cha Golgotha ! [br] 

4. Kisima hicho : Yesu kristo : na maji  damu yake.
Wasumbuka Wastarehe, Waburudishwe hapa! [br] 

5. Na wanye dhambi wanaitwa kwa wingi wa rehema,
Na wakosaji na maskini wasaidiwa sana. [br] 

6. Tumeipata tunu kubwa, Neema kwa neema.
Apokeaye fungu lake, Ni mtu wa uheri. [br] 

7. Heleluya! Tuna’himidi Mwenyezi na Mwanawe
Na Roho takatifu pia. Haleluya! Amina.