110 MWAMBA ulio pasuka

Written by

in

1. Mwamba uliopasuka, ndani yako nijifiche! Maji yale, damu ile itokayo mbavu zako, iwe dawa ya kuponya roho yangu na ubaya!

 

2. Kazi za mikono yangu, haziwezi kukomboa. Hata ningelia sana na kutenda kazi nyingi, singeweza kuokoka, peke yako u Mwokozi.

 

3.Ndani yangu sina kitu, naushika msalaba. Uchi mimi, univike! Sina nguvu, ‘nichukue! Ni mchafu, unioshe! Wewe u Mwokozi wangu.

 

4. Kwa maisha yangu yote hata nitatoa roho, hata saa ya kuitwa mbele ya Mfalme wangu, mwamba uliopasuka, nijifiche ndani yako!

A.M. Toplady, 1776

Video hii wanaimba sauti moja ila maneno tafauti, hii ni version ya Tanzania


 

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com