240 NAVUTWA kwake Yesu na ninamufurahiya

240

1. Navutwa kwake Yesu na ninamfurahia, uzuri wake unapita vyote vya dunia. Siwezi kuupima kweli kwa fikara zangu. Uzuri wake unazidi kuwa bora kwangu!

Siwezi kueleza uzuri wake huku, lakini niaufahamu huko ju’ mbinguni.

 

2. Upendo wa ajabu mno nausifu sana, ukanivuta kwa upole, nije kwa Bwana! Ukaondoa mimi katika unyonge wangu, upendo wake unazidi kuwa bora kwangu!

Siwezi kueleza uzuri wake huku, lakini nitaufahamu huko ju’ mbinguni

 

3. Wokovu wake wakupendwa mno nausifu, uliondoa woga, ukanipa utulivu. Napenda Yesu aliyechukuwa dhambi zangu, wokovu wake unazidi kuwa bora kwangu.

Siwezi kueleza wokovu wake huku, lakini nitaufahamu huko ju’ mbinguni.

W.C. Martin




241 SITASHAWISHIWA tena na dunia huku

 241

1. Sitashawishiwa tena na dunia huku, mema yote ni kwa Yesu, nampenda yeye. Katika safari yangu, Bwana Yesu wimbo wangu. Mbali, kwetu, kila saa namsifu Yesu.

 

2. Mimi mtu heri sana, nampenda Yesu. Vyote nimempa yeye, namtumikia. Tumaini langu kuu nimeweka huko juu. Mbali, kwetu, kila saa namtumikia.

 

3. Njia yote kwenda mbingu nifuate Yesu! Nifanane naye Bwana, niwe nuru huku! Namkiri Yesu pote na katika hali zote! Mbali, kwetu, kila saa nifanane naye!

James Rowe/ Paul Ongman




242 MAISHA yangu yote nimali ya Mwokozi

242

1. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Maungo, roho na akili, yeye ameyabadili. Siku zangu zote ni mali ya Mwokozi.

Pambio
Wakati wangu wote ni mali ya Mwokozi. Machoni pake ni amani, natumika kwa shukrani. Namsifu Yesu, amenihurumia!

 

2. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Naomba niwe mpendevu, nitafute wapotevu! Aliwanunua kwa damu takatifu.

 

3. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Unijalie kati’ mwendo kuongoza kwa upendo wana wapotevu, wapate kuokoka.

 

4. Maisha yangu yote ni mali ya Mwokozi. Nakaa miguuni pake, siku moja huko kwake inapita elfu pengine bila Yesu!

W.C. Martin




243 UKICHOKA kwa safari ngumu

243

1. Ukichoka kwa safari ngumu, sema na Yesu, sema na Yesu! Waogopa kwamba hutadumu, sema na Yesu daima!

Pambio
Sema na Yesu, sema na Yesu, yeye rafiki amini! Akupenda kwa upendo bora. Sema na Yesu kwa yakini!

 

2.Ukilia chozi ya majuto, sema na Yesu, sema na Yesu! Ukiteswa ju’ ya dhambi nzito, sema na Yesu daima!

 

3.Je, wahofu jua likifichwa? Sema na Yesu, sema na Yesu! Kwa taabu ukihuzunishwa, sema na Yesu daima!

 

4.Ukisumbukia kufa kwako, sema na Yesu, sema na Yesu! Ukiteswa kwa maisha yako, sema na Yesu daima! E.S.

Lorenz
Tell it to Jesus, R.S. 592 




244 SAFARI yangu huku ikiwa hatarini

244

1. Safari yangu huku ikiwa hatarini, na ikipita katika giza na jaribu, najua kwa hakika: Mwokozi yu karibu, ninamfuata mahali po pote.

Pambio:
Nikiwa pamoja na Yesu sina hofu. Anipa furaha na heri rohoni mahali pote. Ikiwa nitayashiriki mateso yake, nitamfuata Mwokozi hata mwisho.  

 

2. Nikitangaza neno la Mungu duniani katika mataifa walio wakaidi. Nina furaha kubwa moyoni mwangu, kwani Mwokozi yu nami mahali po pote.

 

3. Na Bwana akitaka nibaki hapa kwangu, wengine wakitumwa mahali pa ugeni, kusudi langu moja: nidumu mwaminifu, na nimfuate mahali po pote!

 

4. Si lazima nijue makusudio yote, ni kazi yangu huku kumfuate yeye. Ikiwa nitabaki, ikiwa nitakwenda, nitamfuata Mwokozi po pote.

C. Austin Miller
It may be in the valley, R.H. 465




245 MIKWAJU itiapo giza na kivuli

245

1. Mikwaju itiapo giza na kivuli katika nchi ya Bersheba ya zamani, alitembea Ibrahimu asubuhi, na maumivu na huzuni ni rohoni, kwa kuwa aliitwa na Mwenyezi Mungu kutii amri yake bila nung’uniko. Na hapo akaomboleza: “E’ Bwanangu, wataka nitakutolea mwana wangu?”

 

2. Sauti ya Bwanake aliifaamu: “Mtwae sasa mwana wako wa pekee, ukamtoe mwana juu ya madh’bahu; kafara ya thamani ukanitolee!” Na moyo wake ukamtulia sana, akitukuza Mungu akitumaini yakuwa yeye atamfufua mwana; alimjuwa yeye aliye mwamini.

 

3. Akaamka Ibrahimu alfajiri, akatandika punda, akatwaa kuni. Pamoja na mwanawe tena ‘kasafiri, na roho yake ikalia kwa huzuni. Mwanawe Isak’ aliyemfurahia: kipeo cha furaha ya uzee wake, matumaini yake yote ya dunia, kafara atakayotoa kwa Bwanake.

 

4. Katika njia ya mlima wa Moriya mtoto akamsaili baba yake: “Tazama moto uko, kuni ziko pia, kondoo mume kwa kafara yuko wapi?” Na Ibrahimu akajibu kwa imani isiyoona shaka wala kudhania: ” Kondoo mume kwa kafara ya shukrani, ninasadiki Mungu atajipatia.”

 

5.Je awezaje Ibrahimu kusahau wakati huo wa uchungu na huzuni, na jinsi akajenga huko madhabahu, na tena akamweka mwana ju’ ya kuni? Akakitwaa kisu amchinje mwana, halafu aliposikia neno tamu:”Usifanyie neno sasa kwa kijana, najua wanipenda sana Ibrahimu!”

 

6. Akainua macho yake kwa haraka, tazama dume la kondoo, nyuma yake, aliyenaswa pembe zake kwa kichaka! Akamtoa akomboe mwana wake. Na malaika akamwita akasema:”Umenitii nami nitakubariki. Na kwa uzao wako mataifa tena wa’barikiwa kwani umenisadiki”.

 

7. Machozi yamekuwa mengi tangu hapo; wakristo wamekamilika kwa jaribu. Na mlimani mwa Moriya wazikapo matumaini yao, pendo na nasibu. Lakini juu ya mlima wa kafara Mwenyezi Mungu abariki watu wake. Awajulisha nguvu zake na ishara, awajaliza Roho ya ahadi yake.

Otto Witt 




246 HESHIMA na sifa zina Baba mbinguni

246

1. Heshima na sifa zina Baba mbinguni, aliyetupenda zamani na sasa!

Pambio
Haleluya, usifiwe! Haleluya, amina. Haleluya, usifiwa! Haleluya, amina.

 

2. Heshima na sifa zina Yesu Mwokozi, alitufilia kwa’jili ya dhambi!

 

3. Heshima na sifa zina Roho wa kweli, anashuhudia Mwokozi na damu!

W.P. Mackay, 1863




247 NAPENDA sana kumushukuru Mwokozi

247

1. Napenda sana kumshukuru Mwokozi wangu kwa nia huru; kwa wimbo wangu nashuhudia upedo wake na damu pia.

 

2. Nikishukuru mateso yake msalabani na kufa kwake, nataka katika wimbo wangu kumtolea shukrani yangu.

 

3. Naimba sasa, nina faraja, katika Yesu nina faraja. Ni mambo tunayofunuliwa, kwa wenye dhambi yamefichwa.

 

4. Kwa neno lake ananiambia kwamba ananihurumia, na ukombozi ninao sasa kwa damu iliyonitakasa.

 

5. Na msione ajabu sana ya kuwa namshukuru Bwana! Ninamwimbia kidogo sasa, ‘taendelea mbinguni hasa.

 

6. Anipa vyote kwa pendo lake, urithi wangu wachungwa kwake hata wakati wakuhamia mbinguni, na nitashangilia.

Anders Nilsoon




248 YESU akiniongoza sitaanguka

248

1. Yesu akiniongoza sitaanguka, sitaanguka. Ni Mfalme mtukufu, Mwokozi wangu, Mwokozi wangu.

Pambio
Wakati huu, hata milele apita vyote vya dunia. Yesu amenichagua, Mwokozi wangu, Mwokozi wangu.

 

2. Yesu amenipa raha, ni kiongozi, ni kiongozi. Anaka’ moyoni mwangu, Yesu Mwokozi, Yesu Mwokozi.

 

3. Nilikuwa kama chungu kilichovunjwa, kilichovujwa. Sasa nimeokolewa na Bwana Yesu, na Bwana Yesu.

 

 4. Nitakapofika mbingu nitamsifu, nitamsifu Yesu kwa upendo wake, Mwokozi wangu, Mwokozi wangu.




249 ZAMANI mjini mwa Yerusalemu

249

1. Zamani mjini mwa Yerusalemu waisrael’ waliabudu. Wakristo wa sasa wanakusanyika kuomba, kusifu Mwokozi.

Pambio:
Msifuni, msifuni Mungu wetu, kwani ametutendea mema! Tutamsifu tu aliyetoka ju’, shangilieni Mwokozi mwema!

 

2. Mwokozi yu nasi, ame’fumbulia uweza wa kutuokoa. Na yu mwaminifu, atusikiliza, apenda kutupa baraka.

 

3. Twaomba baraka na mvua ya mbingu kuithibitisha Injili! Wagonjwa wapone, vipofu waone, Tupate ‘batizo wa Roho!




250 IKAWA siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu

 250

1. Ikawa siku kubwa kwangu aliponiokoa Yesu. E’ roho yangu umsifu Mwokozi wako Yesu Kristo!

Pambio:
Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu! Na kwa neema na upendo akaondoa dhambi zangu! Siku kuu, siku kuu aliponiokoa Yesu!  

 

2.Nimeokoka, nafurahi! Ananitaja mwana wake! Alinivuta kwa upendo, nikafuata mwito wake.

 

3.Ni shangwe ku’ moyoni mwangu nikifuata Bwana Yesu. Anipimia ne’ma sawa wakati wote ma maisha.

 

4. Kwa pendo kubwa na rehema ananitunza siku zote. Sitasaahu siku ile aliyoniokoa Yesu.

Oh, happy day, R.Sl 622; R.H. 619




251 HERI mimi kwani Mukombozi wangu alitoa dhambi

251

1. Heri mimi kwani Mkombozi wangu alitoa dhambi zote! Shangwe na furaha zanijaza mno, kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi!

Kila siku nafurahi! Heri mimi kwani Mkombozi wangu alitoa dhambi zote!

 

2.Heri mimi, Yesu alinifilia; ni furaha ku’; yu hai! Ni rafiki kweli anayetuweka huru toka minyororo.

Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi Yesu alinifilia; ni furaha ku’: Yu hai!

 

3.Heri mimi kwani ananiongoza; nafuata nyayo zake. Nikiyasikia tu maneno yake, sitaweza kupotea.

Kila siku nafurahi! Kila siku nafurahi! Heri mimi kwani ananiongoza, sitaweza kupotea!




252 NINAKUSHUKURU Mungu kwa fadhili

252

1. Ninakushukuru Mungu kwa fadhili zako zote, kwa furaha na uchungu, kwa neema njia yote! Kwa kipupwe na masika, kwa wakati wa machozi. Na kwa raha kadhalika na’shukuru Mkombozi!

 

2. Ninakushukuru Bwana kwa kunifunua siri, kwa kusikiliza sana, ombi na kulifikiri! Na kwa msaada wako, kwa wakati wa jaribu. Kwa agano la Mwanako nashukuru! U karibu.

 

3. Nashukuru wewe pia kwa uzuri wa mbinguni, nuru ulioitia, na kwa jambo la huzuni! Kwa jaribu na kwa giza na kwa siri ya imani, tena kwa kunijaliza ninakuwa na shukrani!

 

4. Kwa waridi za njiani na miiba yao pia, kwa mahali pa amani uliopotuandalia, kwa agano la upendo, kwa kutupa tumaini, kwa kifiko cha mwenendo: Nashukuru! U amini!

Augut Storm, 1891

 




253 SIKU ya furaha inatufikia

253

1. Siku ya furaha inatufikia, siku nzuri katika nchi. Mungu asifiwa mbali na karibu! Malaika wanamshukuru Bwana.

 

2. Huko Bethlehemu alipozaliwa Yesu Kristo Mwokozi wetu, pendo la Mwenyezi likadhihirika; raha ya mbinguni imefika kwetu!

 

3. Ni karama kubwa tuliyoipewa kwa mkono wa Baba Mungu. Roho mfariji anatuongoza, atuonya njia iendayo kwake.

J.D. Falk, 1816
Sweet the moments, rich in blessing, R.S. 566; R.H. 701




254 E’ROHO yangu

254

1. E’ roho yangu, sikiliza vema, wimbo wa juu unatufikia! Shangwe na raha unatuletea, amezaliwa Mkombozi wetu.

Pambio:
Ahimidiwe Mungu wa mbingu! Na duniani iwe raha na amani!

 

2.Ninafurahi kwani wimbo huo tungali tunausikia huku. Na kwa upendo Mungu aita: “Mfike kwangu, nitawapa raha!”

 

3. Katika nchi, mbali na karibu, sauti ya Mwokozi inavuma. Watu wa dhambi wanakuja kwake, awapokea na awaokoa.

F.W. Fabe




255 ZIMETIMIZWA Ahadi njema

255

1. Zimetimizwa ahadi njema: Amezaliwa Mwokozi wetu! Na yote Mungu aliyosema kwa manabii kwa ajili yetu, tumeyapata na kuyaona katika Yesu, mwanawe Mungu. Alitujia na tumepona, twaweza wote kufika mbingu.

 

2. Alijidhili kuwa maskini, na alifika ulimwenguni, Mwokozi wetu, twaiamini. Walimlaza katika hori. Na utukufu kwa Baba yake aliuacha, rehema kuu! Na twende sote horini kwake, tumsujudu aliye juu!

 

3. Mtoto huyo – mfano wetu, si mtu tu, bali Mungu pia. Akawa mwenye kutukomboa, kwa Golgotha alitufilia. Tulipotea vibaya sana katika dhambi na ukaidi, kwa umaskini wa Yesu Bwana twapata kuwa wote tajiri.




256 ASUBUHI na mapema

256

1. Asubuhi na mapema siku ya habari njema twende sote Bethlehemu! Mungu ameturehemu!

 

2.Nyota kubwa inang’aa ju’ ya nyumba ana’kaa Mwana wake wa pekee. Mbele yake tujiweke!

 

3. Wachungaji wasikia nyimbo zao malaika: ” Asifiwe Mungu juu, duniani raha kuu!”

 

4. Mariamu anachoka, safarini wana’toka, analaza mwana ndani ya sanduku la majani.

 

5. Wachungaji wanafika, na magoti wana’piga; waliacha kundi lote kushukuru Yesu wote.

 

6. Mwana yule ni Mwokozi, msaada, Mkombozi. Neno la kuaminiwa, Mungu ametushukia!




257. SIKU ya kuisikia parapanda

257

1. Siku ya kuisikia parapanda yake Mungu, ikiita wateule wake wote, kwa neema tutakaribishwa na Mwokozi wetu katika kutano kubwa huko juu.

Pambio:
Tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake katika kutano kubwa huko juu.

 

2. Mungu anawafufua wafu wake siku ile, na wakristo hai watabadilika, wote watanyakuliwa kumkuta Bwana Yesu, tutakusanyika wote huko juu!

 

3. Wimbo wa mbinguni kama maji utakapovuma, utukufu wake Yesu tuta’ona. Nami pia kwa neema nitafika siku ile kusikia neno lake la “karibu!”

James M. Black, 1893
When the trumpet of the Lord shall sound, R.S. 528




258. MIKUTANO kubwa gani mlimani

258

1. Mkutano ‘kubwa gani mlimani mwa Sayuni asubuhi ya milele? Hawa walinunuliwa tena walitakasiwa, wawe malimbuko kwa Mwokozi.

 

2.Hata kufa huku chini walikuwa waamini, walimfuata Yesu. Sasa wanaka’ mbinguni, wametoka jaribuni, wamerithi raha yakipeo.

 

3.Ukamili wa uzuri wa muziki na zaburi unatoka huko juu! Ni sauti tamu mno ya kinubi na ya wimbo kandokando ya Mwokozi wetu!

 

4. Wimbo huo ni wa nani, wa sauti ya tufani, wa kutia raha kuu? Ndio wimbo mpya ule uimbwao sasa kule ili kuhimidi Mkombozi.

 

5. Bwana, unilinganishe, na ulimi u’safishe, nami nikaimbe huko! Nipe vazi la rohoni, safi sana, la kitani lifaalo asubuhi hiyo!

Carl Boberg, 1884




259. NAFIKIRI siku tutakayofika huko kwetu

259

1. Nafikiri siku tutakayofika mbinguni huko kwetu, na malaika kwa furaha watatukaribisha.

Pambio:
Wataimba wimbo wakutupokea: “Karibuni! Karibuni wote kwetu!” Malaika wa Mungu watatulaki kwa nyimbo za furaha: “Twawasalimu! Karibu kwetu!”

 

2. Mkutano ‘kubwa umekwenda mbele na sasa uko kule. Huimba kwa sauti kuu ukimsifu Mungu.

 

3. Sisi nasi tutakusanyika huko Yerusalemu mpya, na mkutano wa wakristo utatuamkia.

 

4. Bwana Yesu naye atatupokea, atatukumbatia katika nyumba ya mbinguni iliyo ya milele.

Fredrik Engelte




260. MWENYEZI amejenga mji

260

1. Mwenyezi amejenga mji, Mfalme wa huko ni Yesu, Yohana aliouona kushuka kutoka mbinguni. Ukuta ukawa wa jaspi, na njia ya dhahabu safi. Wakati nitakapohama, nitachukuliwa Sayuni.

Pambio:
Mjini mle mtakatifu Yesu atuandalia makao. Sasa nangoja, nautamani mji mzuri kutoka mbinguni.

 

2.Na dhambi hazitafikapo, uchafu hautaingia, mateso, ugonjwa na kufa hazitakuwapo mjini. Na mle tutayasahau mashaka, ‘jaribu na vita; hatutaachana milele. Hakuna uchungu rohoni!

 

3. Mjini hatutayaona kilio na maombolezo. Na huko hatutadanganywa, haitakuwamu husuda. Na wana wa Mungu waona uzuri na utakatifu; nitakapofika mjini nitashangilia daima

 

4. Wapenzi, rafiki na wale waliomaliza safari, watashangilia kabisa kwa’jili ya damu ya Yesu. Na tutawaona mjini katika makao ya raha. Tumaini letu ni hili: Tutakusanyika mbinuni.

 

 




261. MSAFIRI uliye njiani

261

1. Msafiri uliye njiani, watamani nyumba ya babako. Sikiliza nyimbo za mbinguni! U karibu sana kufikako.

Pambio:
Utakuwako huko, katika mkutano wa wakristo huko mbinguni kwa raha ipitayo fahamu? Utakuako huko wakati wa kuimba wimbo mpya wa kumsifu Mwokozi siku zote?

 

2. Sikiliza sasa makengele yapigwayo huko juu kwetu, ili kutuita sisi mbele ya jioni ya maisha yetu!

 

3. Labda siku ile ni karibu nitakapokwenda, nitahama! Sitaona tena majaribu, nitajazwa kwa kumtazama.

 

4. Lango la mbinguni wazi sasa, Yesu amelifungua kwako. Utaweza kuokoka hasa, usiharibishe heri yako!

Josef Rogner, 1921




262. KITAMBO bado – vita itaisha

262

1. Kitambo bado-vita itaisha, kitambo, na dhoruba zitapoa. Na tena nitalaza kichwa changu mbavuni mwake anayenipenda.
:/: Nitaziona raha na amani, mbinguni hazitakuwapo dhambi. :/:

 

2. Kitambo bado- roho yaumizwa, kitambo katika usiku huku. Machozi nina’toka mara nyingi sababu sijaona bado Yesu.
:/: Lakini asubuhi ya milele huko mbinguni sitalia tena. :/:

 

3. Kitambo bado ya kuchoka huku, kitambo, tena nitaona Yesu. Na huru mbali na hatari zote nitastarehe mikononi mwake.
:/: Uvuli wote utaondolewa kwa nuru huko kamilifu kweli. :/:

 

4. Mateso yangu hayadhuru tena, nitasahau yote kwa Yesu. Nikisumbuka mda duniani, mbinguni sitaona shida, kufa.
:/: Na Mungu atafuta kila chozi, ataondoa maumivu yote. :/:




263. ENYI kundi lake Mungu

263

1. Enyi kundi lake Mungu, muda haba mhimili! Kati’ nchi ya milele mtaona raha tele.
:/: Muda haba, muda haba, tena vita itakwisha. :/:

 

2.Usilogwe na dunia, usiache Mungu wako! Katika mabaya, mema ufuate Bwana Yesu.
:/: Siku zote, siku zote! Hivyo utashinda vyote. :/:

 

3.Ukichoka safarini, ukiona njia ndefu na hatari za jangwani, Mungu akuburudisha.
:/: Raha huko, raha huko yatuliza msafiri. :/:

 

4. Kwa imani tunaona nchi yetu ya ahadi. Ni habari nzuri sana: Majaribu yatakoma.
:/: Mbio sana, mbio sana huko ju’ tutaonana. :/:

 

5. Tukiitwa na mauti kwa furaha tutahama. Tulivyovitumaini, ng’ambo huko tutaona.
:/: Heri tele, heri tele: ‘ona raha ya milele! :/:




264. E’MSAFIRI jangwani

264

1. E’ msafiri jangwani, tazama juu mbinguni! Hapo utaona nyota za faraja na tumaini.

Pambio:
Huko hutayaona machozi wala shida. Mungu atatuliza msafiri mbinguni kwake.

 

2.Ukisumbuka gizani katika pepo, dhoruba, bado wakati mfupi, nuru itatokea tena.

 

3.Ukililia wapendwa waliokutangulia, utakutana na wote, hutalia machozi tena.

 

4. Na karibu na Bwana Yesu utastarehe daima, hutakumbuka mbinguni shida, kufa na sikitiko.