319 Nafurahia wokovu niliopata kwa Yesu

1. Nafurahia wokovu niliopata kwa Yesu, nitasifu Mungu wangu daima huko mbinguni. Wokovu niliopewa, na unanirusha juu, kw’ajili ya shangwe kubwa, inayoimba rohoni.

 

2. Silinganishe wokovu wangu na kitu kingine. Kwani vyote vinakosa, bei ya wokovu wangu. Mwokozi alinifia, alinilipia damu, nayo ni ya bei ghali, safi ya Mwana wa Mungu.

 

3. Ninaupenda wokovu, wanitosha kwa matata, kwani Bwana wa wokovu, hakufuata makelele. Aliwaponya wagonjwa, na alifufua wafu, akahubiri injili, alituonyesha njia.

 

4. Ninakusifu Mwokozi, kwani umeniokoa, umenitosha kwa giza, na sasa niko nuruni. Mwenye upendo ni wewe, neema yake ni kubwa, ulinitosha kabisa, katitka pori na giza.

 

TAMBI, Ntoto 1955




320 Mungu aliacha sisi watu wake walimaji kwa dunia

1. Mungu aliacha sisi watu wake walimaji kwa dunia, aliweka mbegu kwa mikono yetu tuzipande katika watu.

Pambio:
Kazi yetu yote itapimwa, mwenye shamba ni Yesu Kristo. Tusishinde huko na mikono bure katika mavuno ya Mungu.

 

2. Hata roho za watu ni ngumu sana usingoje kupanda; tutavuna mavuno kwa furaha tena tutumikie Yesu daima.

 

3. Siku za ujira zinakaribia. Tutapata hukumu, wenye kazi njema watapata sifa; haya itashika wavivu.

Missionnary, 1958




321 Mwokozi mzuri ni Yesu Kristo, ninamshukuru sana

1. Mwokozi mzuri ni Yesu Kristo, ninamshukuru sana. Alinitafuta kwa njia mbaya, ni mali ya Yesu Mwana.

Pambio:
Kwa damu nafunguliwa, kwa damu nafunguliwa. Alitoa yote kwa mimi na wote, kwa damu nafunguliwa.

 

2. Alibeba dhambi msalabani, alitukomboa sote. Barua za deni na mashitaki, alizipasua zote.

 

3. Ni heri kujua makimbilio, wakati wamajaribu. Nashinda kwa nguvu ya damu yake, asanti Mtakatifu.

 

4. Aliteswa sana kwa Getsemane, uchungu aliunywesha. Lakini kwa mwisho msalabani, alisema imekwisha.

Missionnary




322 Nashika njia ya kwenda mbingu

1. Nashika njia ya kwenda mbingu, mimi msafiri duniani, naishi kwa taabu na mateso mengi. Bali nakaza mwendo nifike mbingu.

 

2. Ijapo shida zanizunguuka, mimi msafiri njia, nashika njia nifike mbingu; nitarithi pamoja na Yesu, nitarithi pamoja na Yesu. :/:

 

3. Wenzangu wote wananigombeza na marafiki wananicheka. Nasumbuliwa hata na wanangu, natazama Yesu rafiki Mwema.

 

4. Ninachofanya maishani mwangu, nimpendeze Mungu aliye Mwema. Nijapoteswa, ninatumaini kuingia mbingu, ni nchi ya raha.

 

MUSAFIRI Chidunga Chigangu, 1993

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=t-eACujIe7U?feature=oembed&w=500&h=281]




329 Ewe Mwana wa Mungu, niokoe nami

1. Ewe Mwana wa Mungu, niokoe nami, nikutumikie na niende Sayuni. (2x)

Pambio:
:/: Sifa zina wewe, Sifa zina wewe, Sifa zina wewe, Milele na milele.:/:

 

2. Mavuno ni mengi, watenda kazi ‘chache. Ita wengi Bwana, waingie kazini. (2x)

 

3. Tuombe kwa bidii Bwana wa mavuno, atume watumishi kati shamba lake. (2x)

 

4. Bwana Yesu yu aja, na ujira wake, kulipa watumishi kama kazi zao. (2x)

WATONGOKA Mulonge Erasto, 1964

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=IZbVs56tJFo?feature=oembed&w=500&h=281]




330 Yesu alipoenda alituachia kazi

1. Yesu alipoenda alituachia kazi, na sasa tuifanye, kwani wakati wapita.

Pambio:
Uyainue macho, uyainue macho! Uyainue macho, uyatazame mavuno!

 

2. Usisimame bure, taifa wapotea usiku, wakabili, hakuna atendaye.

 

3. Aliyekwisha ‘lima, atazamapo nyuma hafai utumishi na ufalme wa Mungu.

 

4.Utapokea nini, ‘subuhi ya milele, watakapopata taji watumishi wa’minifu?

WATONGOKA Mulonge Erasto, 1969

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=QUH_Nh9-yaE?feature=oembed&w=500&h=375]




331 Anayeshuhudia kwamba tutafika

1. Anayeshuhudia kwamba tutafika mbingu ni Roho wake Mungu, anayeweka tumaini la kufika mbingu ni Roho wake Mungu. :/: Tumwombe, tumtafute, Ni wetu Yesu alisema :/:

 

2. Roho yule anafanya njia kati vita kali, kuwaendea ndugu, apungungapo mara tunaanza kuogopa na kujihurumia.

 

3.Upendo wako, ndugu uanzapo, kupunguka, ujuwe Roho yule amekwisha kukuacha, pengine mwili wako unaanza kukusonga, tunaye msaidizi.

 

4. Tunakuomba, Bwana Yesu, umtume kwetu, msaidizi huyo wa maisha yetu huku. Tunaingia sasa kati vita duniani, wandugu tumuombe Mungu.

MUBIKWA Onesimo, 1964




332 Sawa na wapitaji wa dunia

1. Sawa na wapitaji wa dunia. Tunapita huzuni na shida. Siku moja tutaongozwa naye, hata huko mbinguni kwa Baba.

Pambio:
Sawa nyota za mbingu tutang’aa, kwa Yesu Mwokozi mbinguni. Tuishike safari kwa nguvu, na kusifu Mwokozi kwa nyimbo.

 

2. Hatushinde katika dunia, kwa kupewa dhahabu na fedha, ila tunatazama shabaha, ni mjini mbinguni kwa Baba.

 

3. Tukikaa nyumbani wala hema. Tangu utoto hata mauti. Tuna ahadi, kuongozwa naye, kwamba tutafikishwa kwa Baba.

MUBIKWA Onesimo, 1963




333 Sisi huku si matajiri, kwani miaka yapita

1. Sisi huku si matajiri, kwani miaka yapita. Mara nyingi twapata shida, kwani miaka yapita. Tukimwamini Yesu na kumtumikia, tutapata thawabu, kwani miaka yapita.

Pambio:
Yapita, yapita, yapita, yapita, tumikieni Mwokozi, kwani miaka yapita.

 

2. Hatutaogopa kitu, kwani miaka yapita. Bali tutafurahi tu, kwani miaka yapita. Dunia ni shida, mashaka na huzuni. Bali tukaze mwendo, kwani miaka yapita.

 

3. Rafiki wanatuacha, kwani miaka yapita. Na safari itaisha, kwani miaka yapita. Tupande mbegu njema, rohoni mwa wenzetu, wengine waokoke, kwani miaka yapita.

 

MUBIKWA Onesimo, 1963




334 Majira yatuonyesha kwamba

1. Majira yatuonyesha kwamba Yesu yu karibu, ahadi sasa zatimia; tujitayarishe mioyoni.

Pambio:
:/: Tujiandae sasa, na tujiweka tayari. :/:

 

2.Dunia yameremeta na kuvuta macho ya wengi, hayo yote yaonyesha kweli, ni ishara za mwisho.

 

3. Tukeshe kati maombi, tutaumaliza mwendo. Yesu ndiye nuru kushinda, tumtegemee yeye.

 

WATONGOKA Mulonge Erasto, 1968




335 Nitafanya nini mimi, siwezi kitu?

1. :/: Nitafanya nini mimi, siwezi kitu?:/: Siwezi kujiokoa, siwezi kujisafisha, siwezi kujigeuza, siwezi kujirefusha, siwezi kujifupisha, na sitajisaidia. Naomba kwake Yesu, anitengeze (sic).

 

2. :/: Nitafanya nini mimi, sijui mtu?: /: Sijui mawazo yake, sifahamu nguvu zake, sijui upendo wake, sijui imani yake, sijui uzuri wake, wala udhaifu wake. Nitaomba kwake Yesu, mwenye hekima, anifahamishe mtu aliyeumba.

 

3. :/: Nitafanya nini na huu mwili wangu? :/: Nasikia, sifahamu, natazama na sioni, naitika na sifanyi, ninatumwa na siendi, na mwili una matata, wachokoza roho yangu. Nitaomba Roho msaidizi wetu. Nitapewa nguvu kwa jina lake Yesu.

 

4. :/: Nitafanya nini mimi niseme vema?:/: Sijui kusema sawa, maneno yaniponyoka, nayo yanachanganyika, mabaya hata mazuri, yote yatoka pamoja, siwezi kuyarudisha. Ninaomba kwake Mungu anisamehe. Nikaseme kila lugha mpya vizuri.

 

5. :/: Roha inapenda kutumikia Yesu? :/: Ni mwili unakataa, unanizuia sana, badala ya kuhubiri, naenda kwa shamba langu, au kwa byashara yangu. Ninapotaka kuomba uvivu unanijaa, kama nataka kuimba watu huja na maneno. Mungu utanisamehe hayo makosa, yananifikia lakini siyapendi.

 

TAMBI Eae Enok Munaongo, 1977




222 BWANA Yesu amesema

1.Bwana Yesu anasema: “Dhaifu wewe sana. Mimi ni mchunga mwema”. Na kwa hiyo namwandama.

Pambio: Yesu alikufa kwa ajili yangu, aliziondoa dhambi, furaha kubwa kwangu!

2.Pendo la Mwokozi wangu limeyeyusha moyo. Ametoa dhambi zangu na kiburi na uchoyo.

3.Sina kitu mkononi cha kunifaidia; udhaifu u moyoni, Yesu ninamlilia.

4.Mungu akisaidia nitamaliza mwendo. “Yesu alinifilia”, nitaimba huko ng’ambo.

5. Siku moja nitafika mbinguni huko juu, nitaimba kadhalika shukrani kuu.

Elvina M. Hall- T.Truvé
Min Jesus säger mig, Sgt. 419; I hear the Saviour, R.H. 198




1 E’YESU mshindaji wa Golgotha

1. E’ Yesus, Mshindaji wa Golgotha, twakusifu!
Bendera ya mapenzi ni Alama ya Kushinda.
Ulichukua dhambi zetu juu ya msalaba wako.
Twakuhimidi, Bwana na Mfalme! Haleluya!

 

2. Twashinda na zaidi ya Kushinda Kati’ yote Kwa
damu yako, Yesu, na Watuinua moyo .
Katika vita na ‘jaribu Twaipeleka kwa Furaha
Bendera yako nzuri ya Kushinda kati’ vita.

 

3. Mbinguni Mkombozi ni Mkuu mwenye sifa.
Aliondoa dhambi kwa Kutufilia wote.
Mwana-Kondoo wake Mungu, Umestahili
kupokea Uweza, utukufu na Heshima.
Heleluya!


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=Yt2dnFzeXI8?feature=oembed&w=500&h=281]




2 KIJITO kiko chenye damu itokayo Mwokozi

1.  Kijito kiko chenye damu Itokayo Mwokozi, Kiwaoshacho wakosao
    :|: Na dhambi na uchafu :|:

2. Msalabani mnyang’anyi Alikiona hima. Mnyonge mimi kama yeye
    :|: Nitakasike pia! :|:

3. Mwokozi wetu, damu yako Daima ina nguvu ya kuokoa wenye dhambi
    :|: Wa makabila yote :|:

4. Kijito hicho cha ajabu Ni tumaini langu upendo wako nausifu,
    :|: Nasifu hata kufa. :|:

5. Nimeamini, naamini Uliyenifilia, Msalabani umetoa
    :|: Maisha yako, Yesu. :|:


 

 




3 KISIMA safi sana chatoka msalaba

1. Kisima safi sana chatoka msalaba, Kimetufungukia, chatusafisha vema.
Twaweza kusikia sauti yake Yesu: ‘’Unifuate sasa kwa kiti cha neema!’’

Refrain:

Kisima cha msalaba, Damu ya Yesu Kristo, Chatusafisha sisi
sote na dhambi na hatia.

 

2. Ufike, mwenye dhambi, krisima ni karibu! Uache dhambi zako,
upumzike hapa! Katika damu yake kabisa utapona,
Tazama msalaba, kisima kitokako!

 

3. Kisima hicho safi cha damu ya Mwokozi kinatutia
afya na nguvu ya kushinda. Mfalme wetu, Yesu, tumhimidi tena!
Furaha yetu yote ni kushukuru Mungu!


 




4 USIKU kabla yakuteswa

1. Kabla ya kuteswa, Yesu Alikusanya wanafunzi wake; Alifahamu kwamba saa yake ya kutolewa ilikaribia.

 

2. Kwa roho aliona gethesemane, Meteso yake na huzuni nyingi;  Zaidi alihofu saa ile, ata’poachwa hata naye Mungu.

 

3. Alitamani saa ya pasaka pamoja na wapendwa wake huku. Katika pendo lake kubwa sana Aliyashinda majaribu yote.

 

4. Akautwa’ mkate, aka’mega, Twaeni, mle, hu’ ni mwili wangu!  Na akawapa wanafunzi wake. Wa heri kila mtu aminiye.

 

5. Ba’daye akawapa na kikombe, Na akasema: Nyweni nyote hiki! Ni damu yangu inayomwagika kwa ondoleo la makosa yote.


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=xaJOREk2_oY?feature=oembed&w=500&h=281]




5 DHAHABU na feza haziniokoi

1. Dhahabu na fedha haziniokoi, Hazina na mali haziponyi roho,
Lakini kwa damu ya Yesu mwokozi nimenunuliwa nipate uhuru.

Refrain :
Nimekombozwa pasipo mali, kwa neema nimeokoka !
Ni bei ghali : kwa damu yake Alilipa deni langu.

 

2. Dhahabu na fedha hazinilipii madeni makubwa ninayo kwa Mungu.
Mwokozi alinikomboa kwa damu nipate wokovu, nitoke dhambini

 

3. Dhahabu na fedha haziufungui Mlango wa ku’karibia mwenyezi,
Lakini kwa damu nimeifikia Neema ya Mungu aliya mkuu.

 

4. Dhahabu na fedha hazinifikishi nyumbani mwa Mungu niliyemwasia,
Lakini nimekombolewa kwa damu, kwa hiyo nitachukuliwa mbinguni.


 

 




6 TWA’SIFU Mungu kwa ajili ya damu takatifu

 1. Twa’sifu Mungu kwa ajili ya damu takatifu,
Inayotosha kuonda makosa yetu yote.
 

2.Wakristo wanakusanyika karibu ya kisima,
hawapunguki kitu kanwe, wakaa kwa Mwokozi.
 

3. Tuimbe duniani pote juu ya pendo kubwa, 
kwa kuwa tumefunguliwa kisima cha Golgotha !
 

4. Kisima hicho : Yesu kristo : na maji  damu yake.
Wasumbuka Wastarehe, Waburudishwe hapa!
 

5. Na wanye dhambi wanaitwa kwa wingi wa rehema,
Na wakosaji na maskini wasaidiwa sana.
 

6. Tumeipata tunu kubwa, Neema kwa neema.
Apokeaye fungu lake, Ni mtu wa uheri.
 

7. Heleluya! Tuna’himidi Mwenyezi na Mwanawe
Na Roho takatifu pia. Haleluya! Amina.

 




7 MWOKOZI ameutimiza wokovu kwa neema kubwa

1. Mwokozi ameutimiza wokovu kwa neem kubwa,
Na juu ya mwamba wa Neno la Mungu Najenga imani.

Refrain:
Aliniokoa kabisa! Kwa damu alinisafisha.
Ninamshukuru Mwokozi kwa sababu Alinikomboa hakika ! 

 

2. Mzigo wa dhambi aliuondoa kwa neema kubwa.
Naona Furaha rohoni kabisa, Amani ya Mungu. 

 

3. Naweza kukaa mweupe rohoni kwa neema kubwa;
Na roho ya Mungu ananiongoza Njiani daima. 

 

4. Karibu na Yesu nalindwa salama Kwa neema kubwa.
Ahadi za Mungu zanipa Furaha iliyo kamili.


 




8 YESU KRISTO asifiwe!

 1. Yesu Kristo asifiwe! Alizichukua dhambi,
Ne’ma inatoka kwake kati’ damu.
Umeosha moyo wako, umekuwa safi,
huru umeondolewa dhambi kati’ damu?

Refrain:
:|: Kati’ damu :|: Umeosha moyo wako, umekuwa safi, huru?
:|: kati’ damu :|: Umcondolewa dhambi kati’ damu?

 

2. Ukilia, ukijuta dhambi hazitoki kamwe;
Haki kweli uta’pata kati’ damu.
Mambo yakusumbuayo Yesu a’ondoa mara,
Unapata ukombozi kati’ damu.

 

3. Yesu atatuchukua arusini mwake huko.
Umevikwa nguo safi kati’ damu?
Je, wajenga ju’ ya mwamba, moyo wako u mzima,
unashinda kila saa kati’ damu?

 

4. Bwana Yesu asifiwe! Aliloa damu yake,
na kwa damu ya thamani tutashinda.
Asubuhi kubwa ile vita itakapokwisha,
tutaimba kwa Furaha ju’ ya damu.

 




9 NAIAMINI damu yako

1. Naiamini damu yako yesu na msalaba wako Yesu.
Mwokozi wangu wa pekee napata yote, Napata yote kwako.

Refrain : 
Uliyoyahidi Na’pata kwa imani.
Huwezi kuniacha mimi, Napata yote kwako
.

2. Kwa damu nimetasika, Namto wa uzima wako
waniletea nguvu tele, napate yote kwako.
 

3. Nafungwa kwa upendo wako, Njiani unaniongoza,
Na katika hatari zote napat nguvu kwako.
 

4. Ninakupenda, Bwana Yesu, Wanisikia niombapo,
Wanipa jibu la mombi Napata yote kwako.





10 DAMU yako yenye baraka inayotuosha makosa

1. Damu yako yenye baraka Inayotuosha makosa.  

Ilitoka musalabani, Bwana YESU, alipokufa alipokufa.  

Nastahili pata hukumu, Na siwezi mimi kujiosha.  

Unioshe katika damu nipate kuwa safi kabisa!

Refrain:
Safi, Safi kweli, Safi, safi kweli!
Unioshe katika damu nipate kuwa safi kabisa!

 

2. YESU ulivikwa miiba, kuangikwa juu ya mti.  

Ulivumilia mateso, Maumivu na majeraha.  

Ninataka kijito hicho N’ende na nikasafishwe sana!  

Unioshe katika damu, Nipate kuwa safi kabisa.

 

mimi mwenye dhambi rohoni nitaona wapi mwokozi?

yesu kwako msalabani naja ninakuamini sasa.

unioshe katika damu nipate kuwa safi kabisa.

 

4. BWANA, nimefika karibu, unilinde kwako,

mille! ufungue kila kikamba, unijaze moyo mwenyewe!

na karibu ya msalaba nitakaa hata kufa kwangu.

unioshe katika damu nipate kuwa safi kabisa.


 




11 IKIWA wananiuliza msingi wa uzima

1. IKIWA wananiuliza msingi wa uzima je?
twahitaji kuongeza kwa kazi yake Yesu?
Kwa uhodari nitajibu: msingi wangu ni wa nguvu,
ni damu yake Yesu Kristo inatosha sana.

 

2 UMWAMBA wa zamani sana, Daima utadumu.
Na hata siku nita’kufa, nitautegemeya.
Nitakapoondoka huku, nitaimbia majeraha
na damu ya mwokozi wangu, Funguo la mbingu.


 




12 KWA badala yangu kweli Yesu alitoa damu

1. KWA badala yangu kweli Yesu alitowa damu.
Mimi huru na ni heri, Bwana Yesu asifiwe!

Refrain:
Yesu alinikomboa, lakini Si kwa dhahabu na mali ya dunia; bali damu ya mwokozi ni malipo kwa ajili yangu, Haleluya!

 

2. Tuinue msalaba, hata wote wataona Mwana wake Mungu,
hapo Alitowa damu yake!

 

3. Dunia kubwa, Yesu kristo! wingi sana wa upendo:
Yesu aliacha mbingu, alitufiliya sote.

 

4. Sitaweza kufahamu Bei ya wokovu wangu, Bali ninajuwa:
Yesu alinikomboa.




13 NANI aweza kuniweka huru?

1. NANI aweza kuniweka huru? ni Yesu mwokozi, Yesu mwokozi!
nguvu kushinda nipate kwa nani? kwa damu ya Yesu mwokozi!

Refrain:
Kuna nguvu, nguvu za ajabu kuu kati damu yake ya mwokozi! Kuna nguvu, nguvu za ajabu kuu kati damu yake Yesu.

 

2. Nitawezaje kuvunja taa? Kwa damu ya Yesu, damu ya Yesu!
Nikaribie kisima cha hai, kisima cha damu ye Yesu.

 

3. Nitawezaje kuoshwa moyoni? Kwa damu ya Yesu, damu ya Yesu!
Nitakasike katika kisima, kisima cha damu!

 

4. Nitawezaje kutenda vizuri? Kwa nguvu za damu ya Yesu, nguvu ya Yesu!
Nitawezaje kufika mbinguni? Kwa nguvu ya damu ye Yesu.


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=cjnuogOvWSI?feature=oembed&w=500&h=281]