89 NAJUA jina moja zuri

 89

1. Najua jina moja zuri, lapita kila jina huku, lanipa raha na amani, na jina hilo Yesu.

Pambio:
Yesu, jina zuri mno! Yesu, unapenda wote, Yesu, tunalindwa vema katika jina lako.

 

2.Napenda jina hilo jema, linanivuta kwake Mungu. Na katika huzuni yangu lanifariji sana.

 

3. Siwezi mimi kueleza uzuri wake jina hili, lakini namwimbia Yesu, nasifu jina lake.

W.C. Martin, 1901
The name of Jesus is so seet, R.S. 4




90 YESU Yesu jina kubwa

90

1. Yesu, Yesu, jina kubwa, nyimbo zao malaika! :/: Limekuwa ndani yangu mto wa furaha bora:/:

 

2.Jina lake kama nyota, linanionyesha njia. :/: Katika jaribu, shida, na usiku duniani. :/:

 

3.Ni mikono ya upendo yenye kunikumbatia. :/: Hapo najificha vema, kama chombo bandarini.:/:

 

4.Jina hilo liwe kwangu, wimbo wa safari yangu! :/: Niletewe wema nalo, toka nchi nzuri juu! :/:

Carl Boberg
Jesus, Jesus, o, Det, Sgt. 256




91 YESU jina ili njema lichukuwe siku zote!

 91

1. Yesu, jina hili jema, lichukue siku zote! Lina raha na faraja, lichukue uendako!

Pambio:
Jina kubwa, jina zuri la matumaini yetu! Jina kubwa, jina zuri la furaha ya mbinguni!

 

2. Lichukue jina hilo, lenye nguvu yakushinda! Ukijaribiwa huku, taja jina lake Yesu!

 

3. Yesu, jina jema mno, latutia shangwe kubwa, ni makimbilio yetu, ngome, msaada pia.

 

4. Na kwa jina lake Yesu kila goti litapigwa, watu wote watakiri kwamba Yesu ni Mfalme.

 

Take the name of Jusus with you, R.S. 465




92 YESU! jina ili ninapita kila jina duniani pote

92

1. Yesu! Jina hili linapita kila jina duniani pote. Yesu, Yesu! Jina hilo ni marhamu iliyomiminwa.

Pambio:
Jina hili ni lenye nguvu ya kuondoa dhambi zangu zote. Yesu, Yesu! Jina hilo lanitia shangwe na furaha.

 

2. Si jingine jina duniani lenye nguvu, kweli na uzima. Yesu, Yesu! Jina hilo waliloimbia malaika.

 

3. Jina hili lina wema mno, limejaza mbingu tangu mwanzo. Yesu, Yesu! Jina hilo, litaimbwa duniani pote.

 

4. Sitaweza kusahahu Yesu, jina lake ni wokovu wangu. Yesu, Yesu! Nitamwona huko kwake tena kwa furaha.




93 SIKU chache

93

1. Siku chache, na tena wakristo watakwenda kumwona Mwokozi, siku chache na wataipewa thawabu na taji ya uzima.

Pambio:
Nangoja sana Bwana Yesu kama zamu angojavyo asubuhi. :/: Kwa dalili zote ninaona sasa kwamba Yesu yu karibu ya kurudi:/:

 

2. Siku chache za vita ya huku, tena Yesu Mfalme atakuja; tutaona furaha na raha, atatupeleka kwake juu.

 

3. Siku chache machozi ya shida, Mungu atayafuta kabisa. Na baada ya siku si nyingi kwa lango nitaingia mbingu.

 

4. Baragumu la mwisho ‘talia, waminifu watachukuliwa; wote wataingia mbinguni kukaa pamoja na Mwokozi.

J.F. Thori




94 LO! nuru inapambazuka

94

1. Lo! Nuru inapambazuka, na vivuli vya usiku vyakimbia; unaulizwa: U tayari? Yesu yuaja upesi!

Pambio:
Na kama vile ‘pepo uvumavyo po pote, habari iendavyo ulimwenguni mwote. Ni neno la furaha, matumaini yetu: Yesu yuaja upesi!

 

2. Vizazi vingi vimefungwa utumwani kwa minyororo migumu; uhuru ni kwa Bwana Yesu, naye yuaja upesi!

 

3.Na watu wengi waamka, nuru ya injili yafukuza giza. Tutatwaliwa ‘ju mbinguni; Yesu yuaja upesi!

C” Hyllestad, 1895




95 NCHI nzuri yatungoja

95

1. Nchi nzuri yatungoja huko juu ya mawingu, watakapokusanyika wateule. Siku zina’tubakia zinapita mbio sana; waminifu watarithi nchi nzuri.

Pambio:
:/: Lo! Ufalme wake Mungu u karibu!:/: Uwe safi, roho yangu, ukakeshe siku zote! Lo! Mfalme wake Yesu yu karibu!

 

2. Twaamini tutaona nchi ile kwa uwazi, tunangoja sana Mkombozi wetu; kwa dalili tunaona siku yake ni karibu; zinatuarifu Yesu aja hima.

 

3. Maandiko yanasema: Mkombozi atakuja, katika mawingu ataonekana. Haleluya! Haleluya! Atafunga yule mwovu, aliyejaribu kutuangamiza.

 

4. Katika kungoja Yesu watu wengi wamechoka; waamshe, uwaonye kwa dalili! Kwani neno lake Mungu latimizwa mbio sana, tunaona kwamba yesu yu karibu.

D.W. Whittle




96 MWOKOZI wetu aliahidi yakwamba atakuja siku moja kutupeleka

96

1. Mwokozi wetu aliahidi ya kwamba atakuja siku moja kutupeleka mbinguni kwake. Yawezekana upesi sana.

Pambio:
Sioni shida, nina amani kwa Mkombozi na damu yake, na Roho yake Mtakatifu ni arabuni ya ‘rithi yangu.

 

2. Wajumbe wengi wa Bwana Mungu watumwa sasa duniani pote. Waitangaza habari njema ya Yesu Kristo na pendo lake.

 

3.Na watu wengi wanaamini, wanaitika mwito wake Mungu. Kwa roho moja twa kaza mwendo, tufikilie thawabu yetu.

 

4. Twakaribia wakati ule wa kuja kwake Bwanda Yesu Kristo; na tujiweke tayari wote kuchukuliwa mbinguni kwake!

S.M. Linder, 1930




97 BADO kidogo juwa litapanda

97

1. Bado kidogo jua litapanda, siku tuta’pofika huko juu. Huko mbinguni tutapumzika na’pata raha na furaha ya milele.

Pambio:
Tutamlaki Bwana Yesu Kristo, aliyetuokoa kweli hapa chini. Huko mbinguni tutamwona yeye, tutamsifu kwa upendo wake ‘kuu.

 

2. Bado kidogo tutaona vyote vitageuka kuwa vipya tena, na hapo, Yesu, Mwokozi wetu, atatufungulia lango la mbinguni.

 

3. Safari yetu ina majaribu, tutafurahi kwa kufika mbingu. Hatutaona giza, shaka tena, Tutamshangilia Mwokozi wetu.

James Rowe




98 SIKU moja tutaona Utukufu wake Yesu

98

1. Siku moja tutaona utukufu wake Yesu, kama nuru ya umeme atakavyoonekana.

Pambio:
Uhubiri neno lake, kwa bidi’ mahali pote! Siku ni karibu sana; Bwana Yesu atakuja.

 

2. Tangu kale tumengoja siku ya uhuru wetu. Hata nguvu ya mauti itaisha siku ile.

 

3.Heri gani ya wakristo kumlaki Bwana yesu! Watavikwa nguo safi huko juu kwa Mwokozi.

 

4. Pasha hi’habari njema, na wagonjwa uwaponye! Uokowe wapotevu! Wende mbio, usikawie!

 

5. Kwa dalili tunaona kwamba Yesu yu karibu, na Mfale atakuja ‘tupeleka kwake juu.




99 SIKU moja nitamuona Bwana Yesu

99

1. Siku moja nitamwona Bwana Yesu uso wake. Na milele kwa furaha nitaka’ karibu naye.

Pambio:
Nitamtazama Yesu ju’ ya nyota zote pia, huko kwa ukamilifu nitajua nguvu yake.

 

2.Hapa ninaufahamu kwa sehemu wema wake, huko nitamtazama na kushiba kwa kuona.

 

3. Shangwe gani kwa Yesu! Shida zote zitaisha, giza haitakuwapo, na huzuni itakoma.

 

4. Yesu atafika mbio, Lo! Mwenyewe atashuka! Tutanyakuliwa juu ili kumlaki Bwana.

 

Face to face with Christ my Saviour, R.H. 781




100 LO! Bendera inatwekwa

100

1. Lo! Bendera inatwekwa, yatutangulia! Tusione hofu, wenzi, twende kwa kushinda!

Pambio:
Bwana Yesu atakuja, tuilinde ngome! Kwa uwezo wake Yesu tutashinda yote.

 

2.Ibilisi azunguka, akitutafuta; anataka tuanguke, tufe, tupotee.

 

3. Vita kubwa, vita kali inaendelea, tuwe watu wa ‘hodari! Twende, tutashinda!

 

4. Basi, kwa bendera yake tunashikamana. Atutie nguvu yake hata kuja kwake!




101 E’MLINZI twauliza: ”Yesu atakuja lini?

101

1. E’ mlinzi, twauliza: Yesu atakuja lini? Asubuhi ya sayuni ni karibu? Tuambie! Msafiri, yainue macho yako, angalia! Asubuhi ni karibu, usimame, usimame!

 

2. Siku heri ya sabato ya milele ni karibu, na dalili yake Yesu hapo itaonekana. Na rohoni tunaona nchi nzuri ya ahadi. Asubuhi ni karibu, na ahadi zatimia.

 

3. Katika Yerusalemu, mji mpya wa mbinguni, Yesu atatumiliki kwa upendo na amani. Baragumu italia, nasi tutaisikia. Yesu ni karibu sana kutukaribisha kwake.

Sidney S. Brewer




102 SAYUNI ulaki Bwanako




103 SIKU kubwa ya mashangilio inatufikia tena




104 LO! horini Bethlehemu




105 WAKATI wa noeli nafika kwenye hori




106 TUIMBE asubuyi iyi juu yasiku manabii Walioitabiri




107 ALIPOTESWA Yesu peke’ katika Gethemani




108 MWANA-KONDOO’ wa Mungu




109 YESU unionye tena msalaba wako

109

1. Yesu, unionye tena msalaba wako! Huo ni kisima safi chenye kusafisha.

Pambio:
Msalaba wako, Yesu, nausifu sana. Yesu, unilinde huko hata nikuone!

 

2.Huko niliona kwanza ne’ma yako kubwa, Nuru ikafika kwangu ‘toka msalaba.

 

3. Yesu, unilinde huko, unifaamishe jinsi ulivyochukua dhambi zangu zote!

 

4.Unilinde siku zote penye msalaba, nikuone, nikupende, sasa na milele!

Fanny Crosby, 1968
Jesus, keep me near the cross, R.S. 390




110 MWAMBA ulio pasuka

1. Mwamba uliopasuka, ndani yako nijifiche! Maji yale, damu ile itokayo mbavu zako, iwe dawa ya kuponya roho yangu na ubaya!

 

2. Kazi za mikono yangu, haziwezi kukomboa. Hata ningelia sana na kutenda kazi nyingi, singeweza kuokoka, peke yako u Mwokozi.

 

3.Ndani yangu sina kitu, naushika msalaba. Uchi mimi, univike! Sina nguvu, ‘nichukue! Ni mchafu, unioshe! Wewe u Mwokozi wangu.

 

4. Kwa maisha yangu yote hata nitatoa roho, hata saa ya kuitwa mbele ya Mfalme wangu, mwamba uliopasuka, nijifiche ndani yako!

A.M. Toplady, 1776

Video hii wanaimba sauti moja ila maneno tafauti, hii ni version ya Tanzania


 




111 E’YESU sitasahau uchungu wako ‘kubwa

111

1. E’ Yesu, sitausahau uchungu wako kubwa, ulipoteswa Gethsemane usiku peke yako.

Pambio:
Mateso uliyoyaona, uchungu na machozi, Usiku ule Gethsemane, Siyasahau kamwe.

 

2.Naona wewe Gethsemane, ulivyoteswa huko kwa ‘jili ya makosa yangu, na kuitoa damu.

 

3.Huzuni nyingi uliona katika teso lako ulipoachwa peke yako na wanafunzi wako.

 

4.Na ukiona roho yangu haina pendo kwako, uniongoze Gethsemane, nione teso lako!

Edward P. Hammond
Tune: O Lord, remember me




112 ULINDE roho na nafsi yangu chini ya damu

 112

1. Ulinde roho na nafsi yangu chini ya damu, chini ya damu! Makosa, hofu na shaka ziwe chini ya damu yako!

Pambio:
Chini ya damu yako, Yesu, ndani ya mto huo safi, unilinde kwa siku zote, chini ya damu yako!

 

2. Makimbilio ya mwenye dhambi, chini ya damu, chini ya damu, ni ukombozi kwa watu wote, chini ya damu yako!

 

3. Nijaze nguvu na pendo lako chini ya damu, chini ya damu, nipate tena kutii wewe chini ya damu yako!

 

4. Amani kubwa moyoni mwangu chini ya damu, chini ya damu, karama zako zanipa raha, chini ya damu yako.

 

5. Nijazwe Roho Mtakatifu chini ya damu, chini ya damu, daima niwe na moyo safi, chini ya damu yako.

 

Lord, keep my soul from day to day,




113 MSALABANI Mwokozi wangu alijitoa kuniokoa

 113

1. Msalabani Mwokozi wangu alijitoa kuniokoa, na damu yake ilimwagika kwa’jili yangu, kunikomboa.

Pambio:
E’ Golgotha, e’ Golgotha, alipoteswa Bwana Yesu! E’ Golgotha, e’ Golgotha, nilipopata raha kweli!

 

2. Na nchi ile ilitetema, mbinguni jua likafunikwa wakati Yesu alipokufa, akichukua hatia yangu.

 

3. Likapasuka pazia lote, kwa hiyo neno limetimizwa. Naona njia ya mbingu wazi: Nikutakaswa kwa damu yake.

 

4. Mwokozi wangu, upendo gani: Uliutoa uzima wako! Kunikomboa ulisikia mateso yote ya msalaba.

William Darwood, 1886
On Calvary’s brow, R.S. 153