1. Pendo la mungu ni kubwa, pasha habari hiyo! pendo la Mungu ni kubwa, mwanzo wa nyimbo zote. malaika waliimba wachunga wakasikia. tunafurahi kujua pendo la mungu ni kubwa.
refrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!
2. Pendo la mungu ni kubwa kwako uliye mbali. pendo la Mungu ni kubwa, anakuhurumia. ukiendee kisima kinachotoka golgotha, utaupata uzima katika pendo la mungu.
Refrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la mungu ni kubwa!
3. Pendo la mungu ni kubwa, latufikisha mbingu, pendo la Mungu ni kubwa, tutafurahi sana! huko hakuna jaribu wala ugonjwa na kufa. tumeokoka sababu pendo la mungu ni kubwa.
Pefrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!
4. Pendo la mungu ni kubwa, pasha habari hiyo! pendo la Mungu ni kubwa, mwanzo wa nyimbo zote. malaika waliimba wachunga wakasikia. tunafurahi kujua pendo la mungu ni kubwa.
Pefrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!
5. Pendo la mungu ni kubwa kwako uliye mbali. pendo la Mungu ni kubwa, anakuhurumia. ukiendee kisima kinachotoka golgotha, utaupata uzima katika pendo la mungu.
Pefrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!
6. Pendo la mungu ni kubwa, latufikisha mbingu, pendo la mungu ni kubwa, tutafurahi sana! huko hakuna jaribu wala ugonjwa na kufa. tumeokoka sababu pendo la mungu ni kubwa.
Pefrain: Pendo kuu, pendo kuu, pendo kuu pendo la Mungu ni kubwa!
1. Yesu ni furaha yangu, amejaa pendo kweli. Anaweza kusimika kila mwenye udhaifu. Ananipa ujasiri, nguvu, raha na faraja. Hata nikionja kufa, Yesu ni mchunga wangu.
2. Nimefungwa na Mwokozi kwa kifungu cha upendo, hata kufa hakuwezi kunitenga naye Yesu. Mimi wake siku zote, ninataka kumtii. Kwa neema nimepona, nisitumikie dhambi.
3. Kwa mikono ya upendo ninakumbatiwa naye, sitaweza kutafsiri pendo lake kubwa kwangu. Napokea nguvu yake, yanijaza moyo wangu. Yesu ananiongoza katika safari yangu.
1. Naona pendo kubwa mno, latoka kwa Mwokozi wangu, ni tele kama maji mengi yatembeayo baharini. Lanitolea tumaini yakwamba nitatiwa nguvu; na niwe mhodari tena kwa pendo kubwa la Mwokozi!
Pambio: Haleluya! Ni pendo kubwa linalotoka moyo wako! E’ Mungu wangu nakuomba: Nijaze pendo lako tele!
2. Na pendo hilo kubwa mno huyaondoa majivuno, na kunifunza haki kweli, uongo wote niuvue! Hunituliza moyo wangu, huruma nayo hunitia. Na sote tuwe na umoja katika pendo la Mwokozi.
3. Nijazwe pendo hilo kubwa, linibidishe siku zote! Rononi niwe na juhudi nitumikie Bwana Yesu! …
Hazina yako ‘nipeleke kwa watu waliopotea, wafahamishwe pendo kubwa ulilo nalo, Mungu wangu!
1. Haleluya! Nafurahi, ninaimba kila siku sifa zake Mungu wangu, aliyeniweka huru. Haleluya! Bwana Yesu aliniokoa kweli! Haleluya! Mimi wake, yeye ni Mwokozi wangu!
2. Heri! Nilieokoka kwa neema yake kubwa ninataka kumsifu Mungu na wokovu wake. Wakinung’unika wote, sitawafuata wao; nitasifu Mungu wangu siku zote na milele.
3. Kama ndege waimbavyo asubuhi bustanini, Na sauti ya mawingu ivumavyo baharini, hivyo nitamshukuru Bwana wangu kwa furaha. Roho yangu itaimba: Haleluya! Sifu Mungu!
4. Haleluya! Furahini mbele yake Mungu wetu! Na watakatifu wote, mwimbieni jina lake! Malaika wote pia, ……msifuni Bwana Mungu! Mbingu zote zitajibu: Haleluya, Haleluya!
1. Nina rafiki mwema, naye alinifilia; alinivuta kwake na amenifanya mpya. Ni mali yake Yesu tu, ninaongozwa naye, alikomboa mimi kwa agano la upendo.
2.Nina rafiki mwema, na aliondoa dhambi, aliniweka huru na kunipa Roho yake. Na vitu vyote ninavyo ninavitoa kwake, maisha yangu ni yake, yaimba sifa zake.
3.Nina rafiki mwema na anayeweza yote, pamoja naye Yesu tu nashinda majaribu, atanitwaa kwake ju’ mbinguni kwa furaha; Nitastarehe katika makao ya milele.
1. Mimi mkristo nita’vyokuwa katika yote mpaka kufa. Mimi mkristo, ‘navyoshuhudu, dunia yote ikinicheka. Mimi mkristo kwa moyo wote sababu ninampenda Kristo, aliyekufa kwa ‘jili yangu. Anastahili kupendwa nami.
2. Mimi mkristo, neema kubwa! Niliokoka kutoka dhambi. Mimi mkristo, hata ikiwa katika shida na mapigano. Mimi mkristo, na ni askari, nafanya vita kushinda dhambi. Akida wangu ni Bwana Yesu, pamoja naye ‘tashinda yote.
3. Mimi mkristo, na ni mgeni, nimeifunga safari yangu; na sitamani yaliyo huku, ninatafuta yaliyo juu. Mimi mkristo na nchi yangu ni huku juu katika mbingu, hamna njaa na shida humo. Wakristo wote washiba mno
4. Mimi mkristo! Ni neno zuri la kufariji moyoni mwangu linanitwaa ju’ ya huzuni, nipumzike kwa Mungu wangu; Mkristo katika kila hali, na nikiitwa na kufa tena, kwa raha kubwa nitakubali kuchukuliwa mbinguni juu.
1. Sasa tayari kwetu siku ya kuokoka, Yesu alitimiza yote msalabani. Wengi wanamjia Yesu Mwokozi wao, wapate kustarehe, wapone nafsi zao.
Pambio: Mwana-kondo’ wa Mungu tunakusifu sana! Uzima uliweka kwa’jili yetu sisi. Umetufanya kuwa mitume yake Mungu. Kati’ majina yote lako ni kubwa mno.
2. Wewe kwa damu yako ulikomboa sisi, na jua la neema linatuangazia. Tumefahamu sasa pendo la Mungu wetu. Damu imetuunga kati’ agano jipya.
3. Njoo upesi nawe uliyesitasita! Mungu atakujaza neema yake kubwa, raha rohoni mwako inayokutuliza, matumaini, nguvu, pendo lililo bora.
H. Schlager, 1925 Speak to my soul, Lord Jesus, R.S. 567