5. Kwa dalili tunaona kwamba Yesu yu karibu, na Mfale atakuja ‘tupeleka kwake juu.
99 SIKU moja nitamuona Bwana Yesu
99
1. Siku moja nitamwona Bwana Yesu uso wake. Na milele kwa furaha nitaka’ karibu naye.
Pambio: Nitamtazama Yesu ju’ ya nyota zote pia, huko kwa ukamilifu nitajua nguvu yake.
2.Hapa ninaufahamu kwa sehemu wema wake, huko nitamtazama na kushiba kwa kuona.
3. Shangwe gani kwa Yesu! Shida zote zitaisha, giza haitakuwapo, na huzuni itakoma.
4. Yesu atafika mbio, Lo! Mwenyewe atashuka! Tutanyakuliwa juu ili kumlaki Bwana.
Face to face with Christ my Saviour, R.H. 781
101 E’MLINZI twauliza: ”Yesu atakuja lini?
101
1. E’ mlinzi, twauliza: Yesu atakuja lini? Asubuhi ya sayuni ni karibu? Tuambie! Msafiri, yainue macho yako, angalia! Asubuhi ni karibu, usimame, usimame!
2. Siku heri ya sabato ya milele ni karibu, na dalili yake Yesu hapo itaonekana. Na rohoni tunaona nchi nzuri ya ahadi. Asubuhi ni karibu, na ahadi zatimia.
3. Katika Yerusalemu, mji mpya wa mbinguni, Yesu atatumiliki kwa upendo na amani. Baragumu italia, nasi tutaisikia. Yesu ni karibu sana kutukaribisha kwake.
Sidney S. Brewer
257. SIKU ya kuisikia parapanda
257
1. Siku ya kuisikia parapanda yake Mungu, ikiita wateule wake wote, kwa neema tutakaribishwa na Mwokozi wetu katika kutano kubwa huko juu.
Pambio:
Tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake, tutakaribishwa kwake katika kutano kubwa huko juu.
2. Mungu anawafufua wafu wake siku ile, na wakristo hai watabadilika, wote watanyakuliwa kumkuta Bwana Yesu, tutakusanyika wote huko juu!
3. Wimbo wa mbinguni kama maji utakapovuma, utukufu wake Yesu tuta’ona. Nami pia kwa neema nitafika siku ile kusikia neno lake la “karibu!”
James M. Black, 1893 When the trumpet of the Lord shall sound, R.S. 528
290. BARAGUMU litalia sana
290
1. Baragumu litalia sana, watu wote watalisikia. Waliokufa watafufuka na wazima watabadilika. :/: Nani anayeweza? Yesu, mweza yote. :/:
2. Na wenye uwezo wa dunia watatetemeka siku ile, na hawataweza kuinuka kutazama uso kama jua. :/: Nani anayeweza? Yesu, mweza yote. :/:
3. Najua Mchunga wangu mwema, anichunga kwa maisha yangu. Na siku ya mwisho nikishinda, sitaona uchungu wa kufa. :/:Nani Mchunga mwema? Yesu, mweza yote. :/:
4. Mbinguni hakitafika kitu cha uchafu, dhambi na kuasi. Wasiomwamini Bwana Yesu, gadhabu ya Mungu yawangoja. :/: Nani atahukumu? Yesu, mweza yote. :/:
5. Mimi Yesu mzabibu kweli, Baba Mungu ndiye mkulima, na ninyi matawi ndani yangu, na hamwezi neno bila mimi. :/: Nani ni mzabibu? Yesu, mweza yote. :/:
7. Nawapenda, mwisho wa upendo, na ninyi mpate kupendana; hivyo mataifa wataona ya kwamba m watu wangu kweli. :/: Nani mwenye upendo? Yesu, mweza yote. :/:
8. Sisi watumishi wake Mungu, tumeacha vyote vya dunia. Tumemchagua Bwana Yesu, tuwekwe kuume kwake Mungu. :/: Tumshukuru nani? Yesu mweza yote. :/: