4 USIKU kabla yakuteswa

1. Kabla ya kuteswa, Yesu Alikusanya wanafunzi wake; Alifahamu kwamba saa yake ya kutolewa ilikaribia.

 

2. Kwa roho aliona gethesemane, Meteso yake na huzuni nyingi;  Zaidi alihofu saa ile, ata’poachwa hata naye Mungu.

 

3. Alitamani saa ya pasaka pamoja na wapendwa wake huku. Katika pendo lake kubwa sana Aliyashinda majaribu yote.

 

4. Akautwa’ mkate, aka’mega, Twaeni, mle, hu’ ni mwili wangu!  Na akawapa wanafunzi wake. Wa heri kila mtu aminiye.

 

5. Ba’daye akawapa na kikombe, Na akasema: Nyweni nyote hiki! Ni damu yangu inayomwagika kwa ondoleo la makosa yote.


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=xaJOREk2_oY?feature=oembed&w=500&h=281]




75 NILIE msafiri

75

1.Niliye msafiri, mgeni duniani; sioni kwangu hapa, ni huko ju’ mbinguni. Ninatamani nami kukaa siku zote pamoja naye Baba katika utukufu.

Pambio:
Kwangu mbinguni, kwangu, uzuri wa binguni wapita yote huku.

 

2. Mwokozi yuko huko, rafiki yangu mwema, aliyenikomboa na ku’chukua dhambi. Na hata nikiona furaha siku zote ningali natamani makao ya mbinguni.

 

3.Na nikipewa huku vipawa vya thamani, na wakiimba nyimbo za kunifurahisha, rafiki wangu wote wakipendeza mimi, ningali natamani makao ya mbinguni.

 

4.Upesi nitaona kifiko cha mbinguni, Mwokozi wangu Yesu atanikaribisha; Na huko nitaona nilivyotumaini, kinubi nita’piga kumshukuru Yesu.

Lina Sandell-Berg, 1868
Home, home, sweet home


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=RMNKXUgJql4?feature=oembed&w=500&h=281]




140 UKICHUKULIWA na mashaka yako

1. Ukichukuliwa na mashaka yako na kuona hufu kwamba utakwama, uhesabu mibaraka yake Mungu, na utashangaa kwa rehema yake.

Pambio:
Uhesabu mibaraka yote Mungu aliyoyakubariki! Ukumbuke mambo yote pia, na utashangaa kwa rehema yake!

 

2. Na ukiudhiwa na huzuni nyingi, ukiona msalaba ni mzito, uhesabu mibaraka kuchwa pia, na kwa moyo wote utasifu Mungu.

 

3. Wengi watamani mali ya dunia; utajiri wako ni Mwenyezi Mungu. Uhesabu mibaraka na kumbuka: Mali haiwezi kufungua mbingu.

 

4. Na katika mambo yote huku chini ukumbuke pendo kubwa la Mwokozi! Na ujumlishe mibaraka yote, tena mwisho atakuchukua kwake!

Johnson Oatman Jr
When upon life’s billows, R.S. 5


[youtube https://www.youtube.com/watch?v=1VWWUGwVSTU?feature=oembed&w=500&h=281]

[youtube https://www.youtube.com/watch?v=-zQDFxB8ZU0?feature=oembed&w=500&h=281]