Tag: wokovu

  • 54 USIOGOPE mateso yako

    54 USIOGOPE mateso yako

    54

    1. Usiogope mateso yako, Mungu anakulinda, bali tazama mapenzi yake,

    Pambio:
    Mungu anakulinda Mungu anakulinda siku kwa siku njiani mwake. Anakulinda salama. Mungu anakulinda.

     

    2.Ukichukuwa mizigo ‘zito, Mungu anakulinda, kati’ hatari za njia yako Mungu anakulinda.

     

    3. Anakumbuka hitaji zako, Mungu anakulinda. Utashiriki ujazi wake, Mungu anakulinda.

     

    4. Katika njia ya migogoro, Mungu anakulinda. Mfunulie fadhaa zako, Mungu anakulinda.

    Cevilla D. Martin, 1904
    Be not dismayed, R.H. 458

  • 186 FANYIA Mungu kazi

    186 FANYIA Mungu kazi

    186

    1. Fanyia Mungu kazi, mbio usiku waja! Mtumikie Mungu siku zako zote! Anza mapema sana, dumu mchana kutwa! Mbio usiku waja, kazi itakwisha.

     

    2. Fanyia Mungu kazi kama kungali jua, usipoteze bure siku zako huku! Uyatimize yote bila kukosa neno! Mbio usiku waja, kazi itakwisha.

     

    3. Fanyia Mungu kazi, saa yapita mbio! Fanya bidii sana kuokoa ndugu! Mtumikie Mungu kwa nguvu yako yote! Mbio usiku waja, kazi itakwisha.

     

    T. Annie L. Coghill, 1854 M. Lowell Mason, 1864
    Work for the night is coming, R.S. 429

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com