141 MWOKOZI wetu anatupa furaha duniani

 

1. Mwokozi wetu anatupa furaha duniani, atuongoza kwa neema na anatushibisha. 

Tazama, yupo pamoja nasi, neema haitaisha kamwe !
Haleluya, haleluya, haleluya amina!

 

2. Ni vema kumupenda mungu aliyetukomboa, vizuri kuwa mtu wake, sitapotea kwamwe.
Furaha yetu itabakia, ikiwa vyote vingetoweka.
Haleluya, haleluya, haleluya amina

 

3. Ikiwa giza mara nyingi, na jua likifishwa, na tukijaribiwa huku, twajua ni kwa muda.
Mbinguni hatutaona kamwe huzuni wala machozi tena.
Haleluya, haleluya, haleluya, amina

 

4. Na tusisumbukie tena chakula wala nyumba, maana vyote twavipata kwa ne’ma yake mungu!
Njiani yote atuongoza, aichukuwa mizigo yetu.
Haleluya, haleluya, haleluya, amina

 

5. Ikiwa vema huku chini kutegemea yesu, furaha gani huko juu kuona uso wake!
Tutaiona furaha tele, nutukufu hautaisha
Haleluya, haleluya, haleluya, amina!

______________________________________________________________________

 

Comments

3 responses to “141 MWOKOZI wetu anatupa furaha duniani”

  1. croyance Avatar

    love this song also

  2. croyance Avatar

    relaxing song excellent

  3. Marlen Avatar
    Marlen

    Nime barikiwa kwa usiku huu kupata nyimbo izi apa.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com