230 GOLGOTHA Mwokozi alitundikwa mtini

Written by

in

230

1. Golgotha Mwokozi alitundikwa mtini kwa’jili ya wote. Na damu akaitoa Mwokozi ili kutangua dhambi.

Penye msalaba nilikombolewa kwa damu ya Yesu iliyotolewa. Mwamuzi mwenyewe alinikomboa, akanilipia deni.

 

2. Golgotha nami nimesulibiwa pamoja na Yesu Mwokozi; na njia kwa Mungu Baba ni wazi, pazia limepasuka.

Nimesulibiwa pamoja na Kristo, na mtu wa kale alikufa hapo. Na mambo ya kale yamekwisha’pita, lo! yote ni mapya sasa!

 

3. Niliunganishwa naye Mwokozi, na sasa ni hai kwa Mungu. Kuishi ni Kristo, siri ajabu, na kufa faida kwangu!

Kwa damu ya Yesu nimetakasika, hatia na dhambi zimeondolewa. Shetani hawezi kunidhuru tena, nimewekwa huru kweli.

Henrik Schlager, 1870-1934

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com