32 HAPO nilikua chini katika dhambi nyingi

Written by

in

32

1. Hapo nilikuwa chini Katika dhambi nyingi, roho yangu iliona kufa na giza tele. Mungu alikisikia kilio changu huko, naye akanipandisha, kuniponya.

Pambio:
:/: Nimeokoka, nimeokoka! Yesu Mwokozi wangu aliniokoa:/:

2. Sasa Yesu amekuwa makimbilio yangu, na upendo wake ‘kubwa uko moyoni mwangu. Ne’ma yake kubwa sana inajaliza roho, niwe mwaminifu kwake siku zote!

3. Ewe, mwenye sikitiko, kuna matumaini: Yesu anakufahamu, atakusaidia. Atakupandisha toka tope la kuteleza, upokee ne’ma yake kwa wokovu!

James Rowe, 1912

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com