45 WAIZRAELI walika’ Babeli utumwani

45

1. Waisraeli walika’ Babeli utumwani, wakawa na huzuni tu kwa ‘jili ya sayuni.

Pambio
Hapo amri ilifika waliweza kuondoka, shangwe gani mioyoni mwao! Walitwaa vinubi vyao, wakaenda wanaimba hadi, hata kurithi nchi yao.

 

2. Vinubi havikubigwa wakati wa utumwa, na walikaa kimya tu mahali pa ugeni.

 

3. Walipotoka Babeli, ikawa kama ndoto; furaha nyingi rohoni, faraja na uheri.

 

4. Mataifa walisema: «Mungu umefanyaje? Watumwa wameondoka, wamewekwa huru»!

 

5. Katika ulimwengu hu’ ni wengi wafungwao. Uhuru ni kwa Yesu tu kwa kila a’miniye.

Pambio:
Ndiye ameleta amri: Tunaweza kuokoka, shangwe ku’kwa kila ‘aminiye! Njoo sasa, twa’ kinubi, tufuate kwa kuimba hata kuirithi nchi yetu!

Werner Skibstedt

Comments

2 responses to “45 WAIZRAELI walika’ Babeli utumwani”

  1. Abel B MAPENZI Avatar

    Tunashukuru kwa kazi nzuri mulio ifikiya ningeshahuri mungeliweka number yenu ya account Bank ili wenye nia nzuri wanaweza wachangia kiasi watakavyo jisikia kutowa li kazi hio ifanyike kwa ufanisi wa uhakika

  2. Nyimbo Za Wokovu Avatar

    Kuhusu muchango wowote munaweza angalia jinsi yakuutoa kwenye page ya Mchango na Mawasiliano. Mungu akubariki ndugu kwa wazo hili nzuri.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com