77 NAIFUATA njia ya ku’fikia mbingu

Written by

in

77

1. Naifuata njia ya kufikia mbingu na mji mwema ule alio’jenga Mungu. Ninasafiri sasa kutoka duniani nifikie nchi hiyo ya raha na uzima.

Pambio:
Naifuata njia ya ku’fikia mbingu na mji mwema ule alio’jenga Mungu.

 

2. Sijauona bado uzuri wake bora wa mji wa mbinguni, usio na machozi; lakini siku moja, kwa shangwe ya milele nitamsifu Yesu katika mji ule.

 

3. Nifikapo mjini, mlango wake wazi, na hapo malaika watanikaribisha; shindano la dunia halitakuwa huko, na nitaona raha milele na milele.

Comments

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com