181 TUTAZAME kule mbele

Written by

in

181

1. Tutazame kule mbele, asubuhi inakuja! Tuamini Mungu wetu, atafanya kazi yake, kufukuza mashetani, kumiliki nchi yote. Tutashinda tukiomba, Mungu anatusikia.

 

2. Tarumbeta linalia, tuamke wote sasa! Mungu wetu anataka sisi sote tutakaswe! Kila mtu awe safi katika kanisa lake! Uliache nung’uniko, utapata nguvu yake!

 

3. Imba ninyi, watu wake, Bwana yu pamoja nasi! Tutashinda majaribu kwa uwezo wake Yesu. Twende tumhudumie kwa kumpa mali yake; hata roho na akili zimtumikie Bwana!

 

4. Watu wengi hawajui njia yakufika mbingu, wanakuwa wamefungwa kwa mikono ya shetani. Twende tukawatafute, tuwavute kwa Mwokozi, na kuomba na kukesha hata kuja kwake Yesu!

Comments

One response to “181 TUTAZAME kule mbele”

  1. Onésime Niyonganyira Avatar
    Onésime Niyonganyira

    Kuna Makosa Machache Mbalimbali

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com