276. MATENDO ya Mungu yapita fahamu

Written by

in

276

1.  Matendo ya Mungu yapita ‘fahamu, ni nani ayaona wazi? Lakini najua mapito ya Mungu kwa mimi yafaa halisi.

 

2.Njiani sijui maana ya yote, lakini nitayafaamu. Kwa nini kuzisumbukia kwa bure taabu na shida za mda?

 

3. E’ Bwana, unayo magari maelfu, na lenye linalonifaa, u’lichagulie mwenyewe, Bwanangu, nifike salama mbinguni!

 

4.Na kama Elia upesi kabisa nitakavyoacha dunia, uchungu na shida za huku ‘takwisha, milele nitashangilia.

 

5. Tutamsujudu Mwokozi daima, kuimba maelfu pamoja: E’ Mungu, u haki na mwenye neema katika shauri na tendo.

 

6.Halafu nangoja kwa uvumilivu kujua maana kwa wazi. Na matumaini ni yenye uzima: Urithi ninao mbinguni.

 

Emil Gustavsson, 1886

Comments

4 responses to “276. MATENDO ya Mungu yapita fahamu”

  1. Daniel RWIMO Avatar
    Daniel RWIMO

    MUNGU Aliye mbinguni astahili kupewa sifa. Bwana Yesu awabariki sana dada.

  2. Nyimbo Za Wokovu Avatar

    Tunashukuru sana, Mungu akubariki pia ndugu Rwimo

  3. Rose Avatar
    Rose

    Mungu awabarikie naeza ku pata book za nyimbo wapi?

  4. Espoir BONDO Avatar
    Espoir BONDO

    Que Le Bon Dieu vous Bénisses mes chère Sœurs.

Leave a Reply

Your email address will not be published. Required fields are marked *

HTML Snippets Powered By : XYZScripts.com